Saturday, July 29, 2017

JINSI YA KUTENGENEZA SABUNI YA MAJI


JINSI YA KUTENGENEZA SABUNI YA 

MAJI



    MAHITAJI  NA  MALIGHAFI


1.                  Sulphonic(LABSA)                                                     
2.                  Slec  
3.                  Pafyumu (lemon)
4.                  Rangi  (kijani/ nyekundu/ blue)
5.                  Chumvi nzuri ya mawe.
6.                  Glycerin
7.                  Soda ash light.
8.                  Formalin  na alka.
9.                  Maji yaliyokuwa safi .
10.              Chombo zaidi ya lita 25.


JINSI YA KUTENGENEZA

1.      Chukua  sulphonic  1 lita moja weka katika chombo chako cha kutengenezea(lita 25) .
2.      Kisha  chukua  slec  yako weka katika kile chombo ambacho uliweka sulphonic  kisha changanya kwa pamoja.

3.      Chukua  soda ash nusu kilo  kisha iloweke katika maji  lita 5 katika chombo kingine pembeni , kisha chukua mchanganyiko wako huo na  mimina  katika chombo chako chenye mchanganyiko wa sulphonic na sles weka maji lita 15 koroga kwa dakika 10 kuwa makini kwasababu utavimba sana.

4.      Kisha weka vijiko vya chai 2 mpaka 3  vya  rangi  kutokana na rangi unayoitaka lakini angalia isizidi sana koroga tena vizuri.

5.      Kisha chukua  glycerin vijiko 2 vya chai kisha weka katika mchanganyiko wako wa sabuni katika chombo chako na mpaka hapo sabuni itaanza kuonekana .

6.      Kisha weka  25ml yani kwa kiasi unachotaka  pafyumu (lemon) , hii itafanya sabuni yako inukie kwa harufu vizuri.

7.      Koroga chumvi ya mawe  pembeni kiasi kidogo tu kama vijiko 6 ya chai kisha mimina katika mchanganyiko wako na malizia kiasi cha maji mpaka kufikia lita 25 ambazo ni wastani  kabisa.
  NB , Chumvi ikizidi itafanya sabuni yako kuwa inachelewa kutoa  povu kwahiyo kuwa makini sana. 

8.      Kisha weka  alka nusu changanya vizuri  na mwisho malizia kwa kuweka formalin kisha koroga tena vizuri. (alka na formalin sio lazima sana hata kama hautavitumia sabuni yako itakamilika na itakuwa poa kwa matumizi ).


ANGALIZO
1.      Mchanganyiko wako utatoa sabuni lita 25 zikizidi hapo zitakuwa sio nzito kwahiyo kuwa makini.
2.      Kuna baadhi ya malighafi ni sumu kwahiyo tumia vifaa vya kujikinga kama  MASKI NA GLOVES.


Tembelea    www.gawazabrain.blogspot.com  NA gawazaTV - youtube kwa mafunzo kwa vitendo.        0684-863138.

kwa matatizo tuwasiliane usisite kwa hili wakati wowote hata kama ni usiku


Sunday, July 16, 2017