Saturday, July 29, 2017

JINSI YA KUTENGENEZA SABUNI YA MAJI


JINSI YA KUTENGENEZA SABUNI YA 

MAJI



    MAHITAJI  NA  MALIGHAFI


1.                  Sulphonic(LABSA)                                                     
2.                  Slec  
3.                  Pafyumu (lemon)
4.                  Rangi  (kijani/ nyekundu/ blue)
5.                  Chumvi nzuri ya mawe.
6.                  Glycerin
7.                  Soda ash light.
8.                  Formalin  na alka.
9.                  Maji yaliyokuwa safi .
10.              Chombo zaidi ya lita 25.


JINSI YA KUTENGENEZA

1.      Chukua  sulphonic  1 lita moja weka katika chombo chako cha kutengenezea(lita 25) .
2.      Kisha  chukua  slec  yako weka katika kile chombo ambacho uliweka sulphonic  kisha changanya kwa pamoja.

3.      Chukua  soda ash nusu kilo  kisha iloweke katika maji  lita 5 katika chombo kingine pembeni , kisha chukua mchanganyiko wako huo na  mimina  katika chombo chako chenye mchanganyiko wa sulphonic na sles weka maji lita 15 koroga kwa dakika 10 kuwa makini kwasababu utavimba sana.

4.      Kisha weka vijiko vya chai 2 mpaka 3  vya  rangi  kutokana na rangi unayoitaka lakini angalia isizidi sana koroga tena vizuri.

5.      Kisha chukua  glycerin vijiko 2 vya chai kisha weka katika mchanganyiko wako wa sabuni katika chombo chako na mpaka hapo sabuni itaanza kuonekana .

6.      Kisha weka  25ml yani kwa kiasi unachotaka  pafyumu (lemon) , hii itafanya sabuni yako inukie kwa harufu vizuri.

7.      Koroga chumvi ya mawe  pembeni kiasi kidogo tu kama vijiko 6 ya chai kisha mimina katika mchanganyiko wako na malizia kiasi cha maji mpaka kufikia lita 25 ambazo ni wastani  kabisa.
  NB , Chumvi ikizidi itafanya sabuni yako kuwa inachelewa kutoa  povu kwahiyo kuwa makini sana. 

8.      Kisha weka  alka nusu changanya vizuri  na mwisho malizia kwa kuweka formalin kisha koroga tena vizuri. (alka na formalin sio lazima sana hata kama hautavitumia sabuni yako itakamilika na itakuwa poa kwa matumizi ).


ANGALIZO
1.      Mchanganyiko wako utatoa sabuni lita 25 zikizidi hapo zitakuwa sio nzito kwahiyo kuwa makini.
2.      Kuna baadhi ya malighafi ni sumu kwahiyo tumia vifaa vya kujikinga kama  MASKI NA GLOVES.


Tembelea    www.gawazabrain.blogspot.com  NA gawazaTV - youtube kwa mafunzo kwa vitendo.        0684-863138.

kwa matatizo tuwasiliane usisite kwa hili wakati wowote hata kama ni usiku


39 comments:

  1. Naomba kujua Lita moja kwa wastani inauzwa being gani

    ReplyDelete
  2. nimeipenda sana hii. asante sana kwa somo zuri

    ReplyDelete
  3. Very interesting ,but put it in english

    ReplyDelete
  4. Imekaa poa sana,wapi yanapatikana hayo material

    ReplyDelete
  5. Slec unaweka kiasi gani mbona hujaonesha

    ReplyDelete
  6. Je hizi malighafi zinapatikana wapi?

    ReplyDelete
  7. Aisee,vijiko 6 vya chumvi nimefanya but nimeingia hasara,coz imebaki kuwa maji kabisa ,naibadilishaje ili iwe nzito???

    ReplyDelete
    Replies
    1. Ikitokea ivo tena iache kwa siku kadhaa itabadilika na kua nzito

      Delete
    2. Ongeza slice kufanya kuwa nzito

      Delete
    3. Kwa Lita 20 chumvi ni 500g yaani kile ki packet kimoja cha chumvi kinachouzwa 500

      Delete
  8. safi sana. kuzaliwa maskini si tatizi, kufa maskini ndiomtatizo. sasa ni watu kuamka na kuukataa umaskini.

    ReplyDelete
  9. Kwa Lita 40 je inakuwaje vipimo vyake na VP kwa chumvi ya unga

    ReplyDelete
  10. Naomba nitumie bro kwenye email yang

    ReplyDelete
  11. Kwa hapo nliv soma naona kam umetengeneza lita 20 na sio lita 25 na vpimo umesem ni lita 25 sas meshindwa kuelewa hapo

    ReplyDelete
  12. Enter your comment...JAMANI HAYO MATERIALS YA KUTENGENEZA YANAPATIKANA WAPI?

    ReplyDelete
  13. jammani material yanapatikana kwenye maduka gani

    ReplyDelete
    Replies
    1. Inategemea na mkoa, ukiyahitaji sana naomba nitafute kwa namba 0788077444 hata mikoani tunatuma

      Delete
  14. Kweli mzee lakini waweza kutumia kiingereza kwa yale majina ya chemicals maana kiswahili kilinipita Left side mzee

    ReplyDelete
  15. Elimu nzuri ya ujasiriamali,mda mwngne tunahitaj kujitoa kwa faida yetu lakn pia na kwa jamii kiujumla.

    ReplyDelete
  16. Utengenezaji wa Sabuni ya maji na shampoo ya nywele ni sawa?
    Nataka kutengeneza shampoo ya nywele?

    ReplyDelete
  17. Material s hayo yanapatikani kwenye maduka gani nipo makambako njombe please naomba msaada nimelipenda someone lako

    ReplyDelete
  18. Moshi kilimanjaro,material tunapata wapi

    ReplyDelete
  19. Ingekuwa vizuri tungejua mahitaji yanapatikana wapi aidha maduka ya kawaida au supermarket ingekuwa fresh Zaid

    ReplyDelete
  20. Kipi kinafanya rangi ichuje (isionekane) baada ya mda flani

    ReplyDelete
  21. hiyo formalin na alika inafanyanga kazi gani , hata isikue na umhimu, mimi nafunga plodder machine kwa Bar soap, na pia natumia mixer to saponify, je inaweza kukuwa rahisi kuitumia formula yako.

    ReplyDelete
  22. naomba kujua kama umetengeneza sabuni na haija zito ila inatoa povu vzuri kabisa nawezaje kuifanya iwenzito ili nisile hasara??

    ReplyDelete